user_mobilelogo

Party Emblem

Party Flag

 

Youth League

Contact us


Communist Party Marxist - Kenya (CPM-K)
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
P.O Box 101011-00101 Nairobi, Kenya.
 

Let's Get Social

          

 

Related Social Links

 Revolutionary Youth League (RYL)
   
 Revolutionary Student Commission
    
 Revolutionary Women League
 Pio Gama Pinto Institute 

Support CPM-K 

membership

Publications

 

 

 Grab a Copy

 

CPM-K Memberships

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Nawasalimu Makada wote wa Chama Cha Kimonunisti Kenya na Wageni wote waalikwa. Siku ya leo ambayo ni siku muhimu sana yakuadhimisha na kuwasherehekea wafanyikazi wote duniani. 

Leo tunajumuika hapa Kisumu lakini sisi ni baadhi tu ya wavujajasho wengi waliojumuika katika kila Pembe ya dunia kusherehekea nguvu Kazi ya wavujajasho duniani.

Lakini, Kuna nini  chakusheherekea kwa  wafanyikazi ? Wakati mabilioni ya wafanyikazi wanaendelea kukandamizwa na mfumo wa kiimla wa ubepari. Mfanyikazi hana chochote chakusheherekea katika jamii yenye inaongozwa na  uimla wa mtaji wakibinafsi dhidhi ya maslahi ya wanaotengeneza mtaji huo.

Jamii yetu imegawanyika baina ya wavunajasho wachache wanao miliki nyenzo za uzalishaji na wanaozitumia kunyonya nguvukazi ya wavujajasho wengi ambao wanaendelea kuishi maisha ya kichochole.

Wafanyikazi wa Kenya kama wafanyikazi wengine wameenedelea kukandamizwa kwa kulipwa Mishahara duni na isiyoweza kukimu mahitaji yao, wafanyikazi wameendelea kufanya kazi masaa zaidi ya yale yanayotakikana na sheria za kufanya kazi duniani. Mazingira yakufanya Kazi yamezorota na wafanyikazi wengi wanapata ajali na hata magonjwa kutokana na Mazingira duni yakufanya kazi. 

Serikali ya Kenya haijaweka mikakati yoyote yakulinda maslahi ya wafanyikazi na hata kuongeza nguvukazi ya taifa lenye lina watu waliohitimu katika tajriba tofauti na ambao bado hawajapata kazi kwa sababu yakutoendeleza viwanda na kilimo ambayo ndiyo nguzo msingi ya nchi yeyote inayotaka kujiendeleza.

Mashirika yakimataifa kama Benki ya Dunia na IMF( International Monetary Fund) yameendelea kushinikiza matakwa ya ulibarali mamboleo ambayo yamekua na madhara makubwa kwa wafanyikazi na maisha ya mvujajasho wa Kenya.

Serikali hii ya kiimla pia imeendelea kusimamisha na kupinga juhudi zozote za wafanyikazi kuungana na kujitetea. Polisi wametumika kuwapiga wafanyikazi wakati wanapo fanya migomo na serikali imekataa kufuata mikataba ya makubaliano na wafanyikazi wa umma.

Vyama vya wafanyakazi na viongozi wa vyama hivi pia wamenunuliwa ili kulegeza kamba katika mapambano ya wafanyikazi. Sisi wakomunisti tukona na jukumu lakuenda miongoni  mwa wafanyikazi hawa na kuwapa mwamko Mpya wa kimawazo ili wabadilishe mambo yalivyo.

Sisi wakomunisti tunafaa kuendelea na kazi yakujenga vyama hivi vya wafanyikazi na kuleta mawazo ya kimapinduzi kwa wafanyikazi ili waelewe   uwezo walio nao. 

 Ingawaje,  vyama hivi vingine vimeshikiliwa na mabepari mchwara wanaotumia uongozi wao ili kuendelea kujinufaisha kibinafsi kama katibu mkuu wa COTU(Confederation of Trade Union) Bwana Francis Atwoli. Viongozi hawa ni kupe wanaonyonya jasho la wafanyikazi wakenya na lazima tuwapinge ki itikadi na tuwang'oe ili turejeshe hadhi ya vyama vya wafanyikazi wakati wa wazalendo kama Makhan Singh, Fred Kubai, Bildad Kaggia na Chege Kibacia.

Wakomunisti pia tunajukumu la kujenga Chama cha Kisiasa cha wafanyikazi CPM-K kwani tunapigana kuchukua uongozi na kujenga uimla wa wafanyikazi dhidhi ya wanaomilki mtaji, hii ndio njia yakujenga mfumo wa usoshialisti ili kuelekea katika mfumo wa kikomunisti ambapo hakuna ukandamizaji baina ya binadamu na binadamu mwingine.

Chama Chetu CPM-K ndicho kitapeleka harakati na gurudumu la wafanyikazi mbele ya mambo mengine ambayo vyama vingine vya wafanyikazi haviwezi kutekeleza. 

Makada wote wa Chama wanajukumu la kihistoria na la kijamii kujenga Chama mahali wanapofanyia kazi ili kuleta mawazo yakimapinduzi kwa wafanyikazi wengine, Chama chetu nicha wafanyikazi na lazima tukijenge miongoni mwa wafanyikazi wenyewe.

Chama chetu kitajaribu kuleta pia Wakulima na wavujajasho wengine katika jamii ili kuikomboa Kenya na dunia kutokana na maovu ya ubepari na ubeberu. Mapigano ya kwanza yakatukua dhidhi ya mabepari wa nyumbani wanaoendeleza maslahi ya mabeberu na mabepari wa nje kwa kufanya kazi ya kibaraka na kutumia vyombo vya dola venye vinamilikiwa na mabepari wa nje ili kukandamiza jamii.

Nawatakia mazungumzo yenye fanaka katika mkutano wa leo wakuadhimisha siku hii na tuendele kujenga Chama cha wafanyikazi.

 

Yadumu Mapambano ya wafanyikazi !!!

Idumu harakati za kujenga Usoshalisti!!!

Kidumu Chama Cha Wafanyikazi CPM-K !!!

Mwaivu Kaluka.

Mwenyekiti Wa Chama Cha Kikomunisti Umaksi - Kenya.

TROTSKY’S  STOCK-IN-TRADE: A COUNTER-REVOLUTIONARY EXPORT UNFIT FOR THE KENYAN M...
02 Feb 2026 12:38

By Mwaivu Kaluka, National Chairperson of the communist Party of Kenya.   Our Party has been subjected to a series of hairbrained slanders and lifeless diatribes from the Trotskyite World Socialist Website(WSWS). Initially, we chose not to respond to their constant attacks because, in most of their publications, they had hardly raised any fundamental questions about Marxism and its political practice. Most of the vitriol attacks were not questions of general principles, and we thought it would be a waste of time to give attention to such Ideologically deranged characters.    What is eve [ ... ]

Read more
CPMK Announces the Formation of a Committee for the Release of Nicolás Maduro Mo...
31 Jan 2026 08:54

CPMK Statement on International Solidarity with Nicolás Maduro Moros and Cilia Flores   By Booker Omole, General Secretary Communist Party Marxist Kenya (CPMK) January 28, 2026   Comrades,   In response to the illegal and brazen actions of United States imperialism against the sovereignty of the Bolivarian Republic of Venezuela, the Communist Party Marxist Kenya (CPMK) takes the initiative to publish the official mailing details for sending letters of solidarity to President Nicolás Maduro Moros and Cilia Flores, whom we recognise as political prisoners of imperialism.   We aff [ ... ]

Read more
Statement of Solidarity with the Islamic Republic of Iran Down with US Imperial...
31 Jan 2026 08:53

  From the Office of the General Secretary Communist Party Marxist Kenya   Booker Omole 30 January 2026   The Communist Party Marxist Kenya speaks at a moment of grave danger and great possibility in world history. The drums of war beat once again. The sanctions tighten once again. The same old empire sharpens its knives once again.   Today the target is Iran. Let us speak plainly and without diplomatic cowardice. Iran is not under attack because it is cruel. Iran is not under attack because it is backward. Iran is not under attack because it has failed its people. Iran is un [ ... ]

Read more
  The Rural Woman: Not to Be Celebrated—But Liberated
24 Nov 2025 06:00

                                                                  peech on the Peasant Women Day, 15th October, 2025. Written by Leon Munala Secretary of The Peasants and Peasant Organization Delivered by Comrade Karimi Wa Kagendo National Organising Secretary, Revolutionary Youth League Comrades, sisters, and fellow workers! Today, the representatives of global capital in their glass palace tells us to celebrate. The United Nations, that grand committee for managing the common affairs of the global bourgeoisie, has  [ ... ]

Read more